Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yafuta chaguzi tano za UVCCM, tatu za UWT zasimamishwa
Habari za SiasaTangulizi

CCM yafuta chaguzi tano za UVCCM, tatu za UWT zasimamishwa

Shaka Hamdu Shaka, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM
Spread the love

 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimefuta chaguzi tano za umoja wa vijana (UVCCM), pamoja na kusimamisha chaguzi tatu za Jumuiya ya Wanawake ya chama hicho (UWT), kutokana na sababu za ukiukwaji wa maadili ikiwemo rushwa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 27 Septemba 2022 na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Shaka Hamdu Shaka, akitangaza maamuzi ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho, jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa ya Shaka, idadi hiyo inaweza kuongezeka kwa kuwa chama hicho kinaendelea kupokea malalamiko kuhusu chaguzi hizo, huku mengine yaliyopokelewa yakiendelea kufanyiwa kazi.

Hata hivyo, hakutaja maeneo ambayo chaguzi hizo zimefutwa na au kusimamishwa.

“Hadi sasa hatuna idadi kamili ya chaguzi zilizofutwa bado mapema sababu tunaendelea kupokea malalamiko na bado tunayafanyia kazi. Mfano mpaka kufikia juzi kwa upande wa vijana chaguzi zaidi ya tano zimefutwa. Kwa upande wa wanawake kuna chaguzi zaidi ya tatu zimesimamishwa,” amesema Shaka.

Aidha, Shaka amesema chaguzi zilizofanyika kupata viongozi wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, hakukuwa na malalamiko mengi.

“Uchaguzi wa vijana na wanawake tunaendelea kufanyia kazi na tunaendelea kufuatilia. Hata hayo matukio yaliyoripotiwa yamechukuliwa hatua kwa wakati. Maeneo yamekuwa na vitendo kinyume na maadili na upangaji safu,” amesema Shaka.

Shaka amesema “Mambo yote haya chama kimeangalia kwa karibu na nataka kuwahakikishia jicho la chama linaangalia kila hatua. Msisitizo wangu kwa upande wa chaguzi zilizoko mbele yetu tunafuatilia sana suala la rushwa.”

Akitangaza maamuzi ya halmashauri hiyo, Shaka amesema imefanya uteuzi wa mwisho wa wagombea katika chaguzi za viongozi wa CCM ngazi ya wilaya, zitakazofanyika tarehe 1 hadi 2 Septemba 2022.

Wakati huo huo, Shaka amesema NEC imeongeza muda wa zoezi la wagombea wa nafazi zake ngazi ya taifa, kuchukua na kurudisha fomu, kuanzia tarehe 1 hadi 5 Oktoba mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!