Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge: Polisi Liwale hawana jengo kwa miaka 47
Habari za Siasa

Mbunge: Polisi Liwale hawana jengo kwa miaka 47

Zubeir Kuchauka
Spread the love

MBUNGE wa Liwale, Zubeir Kuchauka (CCM), amesema Wilaya ya Liwale mkoani Lindi, haina jengo la Kituo cha Polisi kwa muda miaka 47, badala yake limepanga katika jengo la benki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Akizungumza bungeni jijini Dodoma, leo Alhamisi, tarehe 22 Septemba 2022, Kuchauka alihoji kauli ya Serikali kuhusu wilaya hiyo kupatiwa jengo la Kituo cha Polisi.

“Wilaya ya Liwale ina umri wa miaka 47, sasa haijawahi kuwa na jengo la kituo cha polisi, ukiacha lile jengo ambalo wamepanga lilikuwa la benki. Nini kauli ya Serikali kuipatia Wilaya ya Liwale jengo la polisi,” amesema Kuchauka.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini, amesema katika bajeti ya mwaka wa fedha ujao, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo.

“Tunafahamu wilaya kongwe hizi zimekuwa na vituo lakini chakavu sana, sasa kwa bahati mbaya Liwale hawajawahi kuwa nacho. Nimuahidi katika bajeti ijayo tutaweka kipaumbele ili wilaya yako ianze mchakato.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!