Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kamishna Makarani wa ZAECA ajiuzulu
Habari Mchanganyiko

Kamishna Makarani wa ZAECA ajiuzulu

Spread the love

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar (ZAECA), Ahmed Khamis Makarani amejiuzulu. Anaripoti Jabir Idrissa, Zanzibar … (endelea).

Makarani ambaye ni ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisi Tanzania mwenye cheo cha Kamishna Msaidizi – Assistant Commissioner of Police (ACP), ameandika barua ya uamuzi wake huo na kumkabidhi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ambaye ameridhia uamuzi huo.

Taarifa ya kujiuzulu kwa ACP Makarani imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Charles Hillary kupitia taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari jioni leo Ijumaa.

“Rais wa Zanzibar amekubali barua ya kujiuzulu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar,” imesema taarifa hiyo ikieleza kuwa ni hatua inayofuatia kauli ya Rais Dk. Mwinyi kutaka uongozi ujitathmini.

Rais Dk. Mwinyi alitoa kauli hiyo wakati akihutubia hadhara ya viongozi mbalimbali baada ya kupokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Zanzibar (CAG) ya mwaka 2020/2021.

Ripoti hiyo imeeleza kasoro nyingi za matumizi ya fedha za serikali zinazosababisha ubadhirifu wa mamilioni ya fedha.

Rais Dk. Mwinyi akionesha kukerwa na ufisadi serikalini alisema anashangaa kukuta matatizo hayo yanajirudia na hakuna hata mtuhumiwa mmoja aliyefikishwa kwenye vyombo vya kisheria.

Alisema anashangaa kwamba hakuna kesi hata moja iliyopelekwa mahkamani wakati ofisi yake imekabidhi kwa Zaeca ripoti yenye maelezo thabiti ya namna ufisadi ulivofanyika na wahusika kutajwa na baadhi yao kukiri na kurudisha fedha.

“Hatuwezi kuendelea hivi wizi kila mahali na hakuna kesi iliyopelekwa mahkamani… kwa namna hii inabidi ZAECA mjitathimini. Hatuwatendei haki wananchi,” alisema baada ya kusikiliza maelezo ya saa nne mfululizo ya CAG Dk. Othman Abbas Ali akieleza namna mabilioni ya fedha zilivyopotea huku maofisa masuuli wakikosa maelezo ya zilivyotumika.

Written by
Jabir Idrissa

+255 774 226248

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!