Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango atoa somo Wimbo wa Taifa
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango atoa somo Wimbo wa Taifa

Spread the love

MAKAMU wa Rais Dk. Philip Mpango amelazimika kuanza hotuba yake kwa kufundisha wananchi namna ya kusimama wakati wa kuimba Wimbo wa Taifa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Dk. Mpango ametoa somo hilo kwa kile alichodai wakati wa kuimba wimbo wa Taifa ameshuhudia baadhi ya watu wakiwa wamesimama huku mikono ikiwa mifukoni na mwingine akiweka mikono nyuma.

Makamu huyo wa Rais akihutubia leo tarehe 17 Agosti, 2022, katika hafla ya kukabithi magari ya mradi wa kukuza utalii kusini (REGROW), alikatisha hotuba yake na kwenda pembeni mwa podiamu ambapo alionesha wananchi namna ya kusimama wakati wa kuimba wimbo wa Taifa.

Dk. Mpango amesimama wima na kubana mikono yake mbavuni ikiwa imenyooka kuelekea chini na kusema, “hivi ndiyo unapaswa kusimama mikono yako unaibana hapa (anaonesha kwa vitendo). Sasa kuna wengine walikuwa wameweka mikono mifukoni, mwingine kaweka nyuma. Hapana. Huo sio utaratibu na heshima kwa wimbo wa Taifa, naomba kuwasisitiza Watanzania wote kupitia hadhara hii tuziangatie utaratibu na heshima inayotakiwa kwa tunu yetu ya Taifa, wimbo wa taifa ndio unaotutambulisha.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!