Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango atoa somo Wimbo wa Taifa
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango atoa somo Wimbo wa Taifa

Spread the love

MAKAMU wa Rais Dk. Philip Mpango amelazimika kuanza hotuba yake kwa kufundisha wananchi namna ya kusimama wakati wa kuimba Wimbo wa Taifa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Dk. Mpango ametoa somo hilo kwa kile alichodai wakati wa kuimba wimbo wa Taifa ameshuhudia baadhi ya watu wakiwa wamesimama huku mikono ikiwa mifukoni na mwingine akiweka mikono nyuma.

Makamu huyo wa Rais akihutubia leo tarehe 17 Agosti, 2022, katika hafla ya kukabithi magari ya mradi wa kukuza utalii kusini (REGROW), alikatisha hotuba yake na kwenda pembeni mwa podiamu ambapo alionesha wananchi namna ya kusimama wakati wa kuimba wimbo wa Taifa.

Dk. Mpango amesimama wima na kubana mikono yake mbavuni ikiwa imenyooka kuelekea chini na kusema, “hivi ndiyo unapaswa kusimama mikono yako unaibana hapa (anaonesha kwa vitendo). Sasa kuna wengine walikuwa wameweka mikono mifukoni, mwingine kaweka nyuma. Hapana. Huo sio utaratibu na heshima kwa wimbo wa Taifa, naomba kuwasisitiza Watanzania wote kupitia hadhara hii tuziangatie utaratibu na heshima inayotakiwa kwa tunu yetu ya Taifa, wimbo wa taifa ndio unaotutambulisha.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!