Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RPC Muliro: Marufuku mashabiki kwenda na silaha kwa Mkapa
Habari Mchanganyiko

RPC Muliro: Marufuku mashabiki kwenda na silaha kwa Mkapa

Jumanne Muliro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limewaonya Mashabiki wa Soka nchini watakaokwenda Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya mchezo wa Ngao ya Jamii utakaopigwa Jumamosi tarehe 13 Agosti, 2022 na kuwakutanisha watani wa jadi, wasiende na silaha ya aina yoyote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mabingwa wa Soka Tanzania Bara, Young Africans watapapatuana na Simba SC katika mchezo huo ambao utatumika kama ishara ya ufunguzi wa Msimu Mpya 2022/23.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 11 Agosti, 2022 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Muliro Jumanne Muliro amesema shabiki yoyote hataruhusiwa kwenda Uwanja wa Benjamin Mkapa akiwa na silaha isipokuwa vyombo vya dola.

“Katika kuelekea mchezo huo, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam litachukua tahadhari zote za kiusalama kabla, wakati na baada ya mchezo, usalama utaimarishwa kwa kiwango cha juu”

“Ni marufuku kwa Mtu yeyote kwenda na silaha uwanjani isipokuwa vyombo vya dola vyenye jukumu la usalama eneo hilo, tunawatoa hofu Mashabiki watakaofika kushuhudia mchezo huo kuwa ulinzi ndani na nje ya uwanja utakuwa umeimarishwa kwa kiwango cha juu” amesema Kamanda Muliro

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!