Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko RPC Muliro: Marufuku mashabiki kwenda na silaha kwa Mkapa
Habari Mchanganyiko

RPC Muliro: Marufuku mashabiki kwenda na silaha kwa Mkapa

Jumanne Muliro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limewaonya Mashabiki wa Soka nchini watakaokwenda Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya mchezo wa Ngao ya Jamii utakaopigwa Jumamosi tarehe 13 Agosti, 2022 na kuwakutanisha watani wa jadi, wasiende na silaha ya aina yoyote. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mabingwa wa Soka Tanzania Bara, Young Africans watapapatuana na Simba SC katika mchezo huo ambao utatumika kama ishara ya ufunguzi wa Msimu Mpya 2022/23.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 11 Agosti, 2022 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Muliro Jumanne Muliro amesema shabiki yoyote hataruhusiwa kwenda Uwanja wa Benjamin Mkapa akiwa na silaha isipokuwa vyombo vya dola.

“Katika kuelekea mchezo huo, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam litachukua tahadhari zote za kiusalama kabla, wakati na baada ya mchezo, usalama utaimarishwa kwa kiwango cha juu”

“Ni marufuku kwa Mtu yeyote kwenda na silaha uwanjani isipokuwa vyombo vya dola vyenye jukumu la usalama eneo hilo, tunawatoa hofu Mashabiki watakaofika kushuhudia mchezo huo kuwa ulinzi ndani na nje ya uwanja utakuwa umeimarishwa kwa kiwango cha juu” amesema Kamanda Muliro

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!