Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafugaji nyuki watakiwa kutumia zana za kisasa
Habari Mchanganyiko

Wafugaji nyuki watakiwa kutumia zana za kisasa

Spread the love

WAFUGAJI wa Nyuki nchini wameshauriwa kutumia zana za kisasa katika ufugaji wa nyuki na kuandaa asali ili kupata bidhaa yenye ubora. Anaripoti Selemani Msuya, Mbeya… (endelea)

Ushauri huo umetolewa na Mtaalam wa Ufugaji Nyuki kutoka Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi veta Dakawa mkoani Morogoro Theodora Kiyungu wakati akizungumza na mwandishi wa Mwanahalisi Online, alipotembelea banda la VETA lililopo katika Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.

Mtaalam wa Ufugaji wa Nyuki kwa njia ya kisasa kutoka Chuo cha VETA Dakawa, Theodora Kiyungu akionesha asali bora na nta.

Kiyungu amesema wafugaji wengi wa nyuki nchini wanatumia mbinu za kizamani katika ufugaji na uchakataji wa asali hali ambayo inasababisha thamani ya bidhaa hiyo kushuka.

Mtaalam huyo alisema wapo wafugaji wa nyuki ambao wanachakata asali kwa kutumia chandarua hali ambayo ni hatari kwa afya ya watumiaji.

Amesema VETA Dakawa wanatoa mafunzo ya namna ya kufuga nyuki na kuchakata asali ambayo inakubalika katika soko la ndani na nje.

Pia alisema wanatumia bomba la kisasa kwa ajili ya kutoa moshi na kuwataka wafugaji kuacha kutumia kuni kama njia ya kufukuza nyuki ili kuvuna asali.

“Zao la asali ni moja ya zao muhimu na linalotumika duniani kote, hivyo ni lazima utaratibu wa ufugaji na uchakataji uwe wa kisasa na unaofaa kwa matumizi ya binadamu. Sisi tunaamini wafugaji wakija VETA Dakawa watapata mafunzo sahihi,” alisema.

Alisema pamoja na kupata asali ambayo inatumika kwa jamii, pia kupitia asali wanaweza kupata nta kwa ajili ya utengenezaji wa mishumaa na bidhaa nyingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!