Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafugaji nyuki watakiwa kutumia zana za kisasa
Habari Mchanganyiko

Wafugaji nyuki watakiwa kutumia zana za kisasa

Spread the love

WAFUGAJI wa Nyuki nchini wameshauriwa kutumia zana za kisasa katika ufugaji wa nyuki na kuandaa asali ili kupata bidhaa yenye ubora. Anaripoti Selemani Msuya, Mbeya… (endelea)

Ushauri huo umetolewa na Mtaalam wa Ufugaji Nyuki kutoka Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi veta Dakawa mkoani Morogoro Theodora Kiyungu wakati akizungumza na mwandishi wa Mwanahalisi Online, alipotembelea banda la VETA lililopo katika Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.

Mtaalam wa Ufugaji wa Nyuki kwa njia ya kisasa kutoka Chuo cha VETA Dakawa, Theodora Kiyungu akionesha asali bora na nta.

Kiyungu amesema wafugaji wengi wa nyuki nchini wanatumia mbinu za kizamani katika ufugaji na uchakataji wa asali hali ambayo inasababisha thamani ya bidhaa hiyo kushuka.

Mtaalam huyo alisema wapo wafugaji wa nyuki ambao wanachakata asali kwa kutumia chandarua hali ambayo ni hatari kwa afya ya watumiaji.

Amesema VETA Dakawa wanatoa mafunzo ya namna ya kufuga nyuki na kuchakata asali ambayo inakubalika katika soko la ndani na nje.

Pia alisema wanatumia bomba la kisasa kwa ajili ya kutoa moshi na kuwataka wafugaji kuacha kutumia kuni kama njia ya kufukuza nyuki ili kuvuna asali.

“Zao la asali ni moja ya zao muhimu na linalotumika duniani kote, hivyo ni lazima utaratibu wa ufugaji na uchakataji uwe wa kisasa na unaofaa kwa matumizi ya binadamu. Sisi tunaamini wafugaji wakija VETA Dakawa watapata mafunzo sahihi,” alisema.

Alisema pamoja na kupata asali ambayo inatumika kwa jamii, pia kupitia asali wanaweza kupata nta kwa ajili ya utengenezaji wa mishumaa na bidhaa nyingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!