Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Waziri Ummy aipiga ‘stop’ NHIF
Afya

Waziri Ummy aipiga ‘stop’ NHIF

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

WAZIRI wa Afya nchini Tanzania, Ummy Mwalimu amesitisha mara moja utaratibu mpya wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) unaoweka ukomo wa mahudhurio ya mgonjwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mfumo huo ambao ulianza kutumika rasmi Agosti Mosi, 2022 pia unavitaka vituo vya kutoa huduma za afya kuwa na kibali kwanza kabla ya kutoa huduma kwa mteja wa NHIF kwa vipimo vya MRI, CT SCAN, Colonoscopy, HBA 1C, OGD, USS na ECHO.

Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Jumatano tarehe 3 Agosti, 2022 na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Catherine Sungura, Waziri Ummy ameitaka NHIF pamoja na dhamira nzuri ya kutaka kudhibiti udanganyifu, kukutana kwanza na wadau ili kuja na namna bora zaidi bila kumuathiri mteja na vituo vya huduma.

“Wizara inapenda kuwahakikishia wanachama wa NHIF na wananchi kwa ujumla kuwa itafanyia kazi mapendekezo yote yatakayotolewa na kuja na njia nzuri ili kutimiza dhamira ya Serikali ya utoaji wa huduma za afya kuanzia vituo vya afya ngazi ya msingi hadii Taifa,” ameeleza taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

error: Content is protected !!