Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia: Tutanunua vifaa vya treni vipya, mtumba
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia: Tutanunua vifaa vya treni vipya, mtumba

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imetoa fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya treni ya kisasa, huku akisema miongoni mwa vifaa hivyo vitakuwa vilivyotumika. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Mkuu huyo wa nchi ametoa kauli hiyo leo Jumatatu, tarehe 4 Julai 2022, akishuhudia hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), kipande cha nne kutoka Tabora hadi Isaka.

Rais Samia amesema, miongoni mwa vifaa vipya ambavyo Serikali imeweka oda kiwandani kwa ajili ya kutengenezwa, ni seti za treni za kisasa 10, vichwa vya treni vipya 17 na mabehewa ya abiria.

“Matarajio yangu kuanzia katikati ya 2023, baadhi ya hivi vitu kama sio mwishoni mwa mwaka huu, vingi tumekuwa tumevipokea na vingine tutakuwa tumevipokea 2023. Kwa nini? Kwa sababu vingi vitu tumeagiza,” amesema Rais Samia na kuongeza:

Rais Samia amesema “vipo vya kutengeneza, tutanunua vya kuanzia vilivyotumika lakini vyenye hali nzuri. Tutatengeneza ili reli ifanye kazi lakini tutakavyoviagiza tutavipokea  2023 na vitafanya kazi kwa muda mrefu zaidi.”

Aidha, Rais Samia ameliagiza  Shirika la Reli Tanzania (TRC), kuweka mipango ya biashara ili fedha zipatikane kwa ajili ya kulipa mkopo uliochukuliwa kwa ajili ya kuijenga. Reli hiyo inajengwa kwa gharama ya Sh. 16 trilioni.

“Tuhakikishe tunakuwa na mipango mizuri ya biashara hii ya usafirishaji. Tumeona vichwa vinapita na matumaini yetu kuanzia pengine mwakani katikati, Juni au Julai tutaanza kusafiri kutoka Dar es Salaam hadi Dodom, tuanze kuweka mipango ya kibiashara ya reli ili fedha iweze kurudi na kurudi kwa haraka ili  tuweze kulipa mkopo kwa haraka,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema, ujenzi wa reli hiyo utasaidia kuunganisha mikoa tisa, ikiwemo Dar es Salaam, Morogoro, Singida, Tabora na Simiyu, pamoja na nchi jirani za Uganda, Burundi, Rwanda na Sudani Kusini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!