Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Samia: Si matumani yetu kuona mifarakano nyumba za Mungu
Habari Mchanganyiko

Samia: Si matumani yetu kuona mifarakano nyumba za Mungu

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameonesha kusikitishwa na mifarakano inayotokea katika nyumba za ibada baina ya viongozi wa dini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kagera … (endelea).

“Mnakuwa na mifarakano watu wanagombana wanafika kuchukuliana hatua kubwa,” amesema Rais Samia leo Ijumaa tarehe 10 Juni, 2022 ikiwa ni siku chache tu tangu viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde kufikishana Mahakamani kutokana na migogoro baina yao.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa msikiti uliojengwa na Jumuiya ya Istiqaama mjini Bukoba mkoani Kagera, Rais Samia amesema katika maeneo mengine inazuka mifarakano misikiti inapojengwa hasa ikiwa na vitega uchumi.

Amesema mifarakano inatokea katika kutaka madaraka ya kusimamia na kuendesha misikiti, “hasa kunapokuwa na vibiashara vya kuleta riziki kwenye msikiti huo.”

“Si matumaini yetu kusikia kuna mifarakano kwenye nyumba za ibada, kwenye nyumba za kuabudu Mungu, mnakuwa na mifarakano watu wanagombana wanafika kuchukuliana hatua kubwa, si matumaini yetu kuona mnaelekea huko,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!