Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Samia: Si matumani yetu kuona mifarakano nyumba za Mungu
Habari Mchanganyiko

Samia: Si matumani yetu kuona mifarakano nyumba za Mungu

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameonesha kusikitishwa na mifarakano inayotokea katika nyumba za ibada baina ya viongozi wa dini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kagera … (endelea).

“Mnakuwa na mifarakano watu wanagombana wanafika kuchukuliana hatua kubwa,” amesema Rais Samia leo Ijumaa tarehe 10 Juni, 2022 ikiwa ni siku chache tu tangu viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Konde kufikishana Mahakamani kutokana na migogoro baina yao.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa msikiti uliojengwa na Jumuiya ya Istiqaama mjini Bukoba mkoani Kagera, Rais Samia amesema katika maeneo mengine inazuka mifarakano misikiti inapojengwa hasa ikiwa na vitega uchumi.

Amesema mifarakano inatokea katika kutaka madaraka ya kusimamia na kuendesha misikiti, “hasa kunapokuwa na vibiashara vya kuleta riziki kwenye msikiti huo.”

“Si matumaini yetu kusikia kuna mifarakano kwenye nyumba za ibada, kwenye nyumba za kuabudu Mungu, mnakuwa na mifarakano watu wanagombana wanafika kuchukuliana hatua kubwa, si matumaini yetu kuona mnaelekea huko,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!