Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe azungumzia Rais Samia kutinga uzinduzi kitabu cha Sugu
Habari za Siasa

Mbowe azungumzia Rais Samia kutinga uzinduzi kitabu cha Sugu

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama cha Chadema, Freeman Mboiwe, amesema hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuzindua kitabu cha msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop Tanzania, Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu, ni sehemu ya safari ya nchi katika kufikia mshikamano. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mbowe ametoa kauli hiyo jana Jumanne, tarehe 31 Mei 2022, katika uzinduzi wa kitabu hicho chenye jina la Muziki na Maisha from the street, uliofanyika kwenye tamasha la Dream Concert, Serena Hotel, jijini Dar es Salaam.

“Siwezi kusema ni mwanzo mzuri kwa sababu tayari tumeshakutana na tutaendelea kukutana na kutoa taarifa hatua kwa hatua kwa namna ambavyo tunaendelea kukutana. Lakini ni sehemu ya safari na tumeonesha kwamba we are serious katika hili,” amesema Mbowe.

Mwenyekiti huyo wa Chadema, amewaomba Watanzania wamalize tofauti zao na kuijenga Tanzania.

“Ni matumaini yangu kwamba Watanzania wote wenye kupenda mshikamano katika taifa letu, wataona umuhimu wa kumaliza tofauti zetu na kuijenga Tanzania iliyokuwa na ushirikiano bora zaidi,” amesema Mbowe.

Tangu alivyoingia madarakani Machi 2021, kufuatia kifo cha mtangulizi wake, aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magifuli, Rais Samia amekuwa na desturi ya kutafuta maridhiano na makundi mbalimbali, ikiwemo vyama siasa na viongozi wa dini.

Rais Samia ameshafanya mazungumzo na Mbowe mara mbili, Ikulu ya Dar es Salaam, pamoja na viongozi wa Chadema, Chama cha Wananchi (CUF) na ACT-Wazalendo.

Katika kutafuta maridhiano, Rais Samia ameunda kikosi kazi maalumu kwa ajili ya kukusanya maoni ya wadau kwa ajili ya kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa, ikiwemo marekebisho ya katiba, tume za uchaguzi na shughuli za kisiasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!