Tuesday , 30 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Diwani CCM aliyetoweka akutwa kwa mwanamke akiwa amelewa
Habari MchanganyikoTangulizi

Diwani CCM aliyetoweka akutwa kwa mwanamke akiwa amelewa

Diwani wa Kata ya Kawe, Mutta Rwakatare (CCM)
Spread the love

 

DIWANI wa Kata ya Kawe, Mutta Rwakatare (CCM), aliyetoweka tangu Februari 2022, amepatikana akiwa katika hali ya ulevi kwenye nyumba ya rafiki wake wa kike aliyefahamika kwa jina la Ashura Matitu, maeneo ya Tabata, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 24 Mei 2022 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ACP Jumanne Muliro, ikiwa imepita siku tano tangu Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Songoro Mnyonge, kuliomba Jeshi la Polisi, limsake diwani huyo akidai alifichwa kusikojulikana.

“Jeshi la Polisi lilifanya ufuatiliaji wa taarifa hizo na kufanikiwa kumpata tarehe 23 Mei 2022, akiwa kwenye nyumba ya mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Ashura Ally Matitu, kabila la mzaramo, mkazi wa Tabata.

“Mwanamke huyo alidai diwani huyo ni rafiki yake wa siku nyingi kwa zaidi ya miaka 10 na alifika nyumbani kwake tarehe 19 Mei 2022, huku akiwa katika hali ya ulevi uliopindukia,” imesema taarifa ya Kamanda Muliro.

Taarifa ya Kamanda Muliro imesema, kutokana na diwani huyo ambaye ni mtoto wa marehemu Mchungaji Getrude Lwakatare, kukutwa katika mazingira ya ulevi, Jeshi la Polisi lilimkabidhi kwa ndugu zake kwa ajili ya matibabu.

“Kutokana na mazingira ya ulevi ambayo diwani huyo amekutwa nayo na maombi yaliyotolewa na ndugu zake kwa Polisi kwa ajili ya matibabu.

“Pia kutokana na kumbukumbu za nyuma, mwenendo na tabia za diwani huyo, Polisi limemkabidhi kwa ndugu zake kwa matibabu na tiba zaidi za kisaikolojia,” imesema taarifa ya Kamanda Muliro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!