Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari Marekebisho sera ya elimu, mitaala kukamilika Desemba 2022
HabariHabari Mchanganyiko

Marekebisho sera ya elimu, mitaala kukamilika Desemba 2022

Spread the love

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolph Mkenda, amesema marekebisho ya sera ya elimu na mitaala, yatakamilika Desemba 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Prof. Mkenda ametoa taarifa hiyo katika sherehe za kilele cha wiki ya ubunifu kitaifa, zilizofanyika leo Alhamisi, tarehe 19 Mei 2022, jijini Dodoma.

Waziri huyo wa elimu amesema, hadi itakapofika Septemba 2022, taarifa kuhusu mabadiliko hayo zitafikishwa kwa viongozi wakuu wa nchi.

“Katibu Mkuu wa UN ameita kikao cha wakuu wa nchi jijini New York, Marekani Septemba mwaka huu kuzungumzia masuala haya ya mageuzi katika elimu. Bahati nzuri sisi tumeshatangulia kwa sababu Rais wetu alishatuelekeza kufanya kazi hiyo. Nadhani itakapofika Septemba tutakuwa tumeshatoa briefings kwa wakuu wa nchi,” amesema Prof. Mkenda na kuongeza:

“Tuko tayari kukamilisha kazi yote tukifika Desemba ili mwakani wakati dunia inafanya mchakato sisi tumeshafanya maamuzi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari Mchanganyiko

Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba

Spread the love MKUU wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Kennan Kihongosi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

error: Content is protected !!