MBUNGE wa Nzega Vijijini, Dk. Hamisi Kigwangalla (CCM), ameishauri Serikali ibadili mfumo wa utoaji ajira za watumishi wa umma, akitaka iajiri watu kutoka maeneo yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).
Dk. Kigwangalla ametoa ushauri huo leo Alhamisi, tarehe 19 Mei 2022, akizungumza katika ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan, mkoani Tabora.
Mbunge huyo wa Nzega Vijijini, ametoa ushauri huo akizungumzia ajira zilizotangazwa na Serikali hivi karibuni, zaidi ya 10,000.
“Tunafahamu utaratibu wa kawaida watoto wataajiriwa central halafu watasambazwa kwenye maeneo yenye uhitaji nchi nzima. Sisi tunaomba kuwe na usawa kwenye kugawa nafasi za ajira wachaguliwe kutoka katika eneo wanalotoka katika majimbo yao,” amesema Dk. Kigwangalla.
Dk. Kigwangalla amesema “kama ambavyo mmetugawia pesa za barabara kwenye kila jimbo, basi hivyo hivyo na nafasi za ajira zigawanywe kwa usawa kutokana na vigezo mbalimbali ambavyo Serikali haitashindwa kuweka.”
Katika hatua nyingine, Dk. Kigwangalla ameiomba Serikali ikamilishe ujenzi wa miradi ya maendeleo, iliyoanza kujengwa jimboni mwake.
Leave a comment