Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mpina ataka Bunge lichunguze majadiliano sakata makinikia
Habari za Siasa

Mpina ataka Bunge lichunguze majadiliano sakata makinikia

Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Luhaga Mpina
Spread the love

MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina ameliomba Bunge kuunda kamati ya kiuchunguzi ili kujua sababu ya Kamati ya Majadiliano ya Kesi ya Makinikia kukubali kupokea Sh 692 Bilioni tofauti na ushauri wa Mahakama ambazo zilisema Serikali inaweza kupata Sh. 6.5 trilioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mpina ametoa hoja hiyo leo Alhamisi tarehe 28, 2022 wakati akichangia majadiliano ya bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria iliyowasilishwa bungeni.

“Mahakama za bodi za rufaa za kodi pamoja na bazara zilisema Trlioni 5.65 zinaweza kupatikana kama kodi lakini kwanini tupate Bilioni 692, ningeomba eneo hili linachangamoto na ningeshauri bunge liunde Tume Teule ya Bunge iende ikachunguze hili kwanza negotuon timu ilifikiaje maamuzi ya kupokea fedha hizo na uhalali wa majadiliano hayo n akile kilichopatikana

Alisema ukiondoa kesi za makinia kuna kesi za Sh Trilioni 5.19 za makosa mbalimbali na kwamba sasa hivi rufaa za kodi zinafikia Trlioni 2 kwa mwaka.

“Tukiruhusu haya kila siku wafanyanbiashara watakuwa wanatukatia rufaa na tutakuwa tunakosa fedha kama kesi hazisikilizwi kwasababu mabaraza hayana fedha au hayana watumishi ni jambo ambalo hakliingii akilini,” amesema Mpina.

Mpina amezungumzia pia namna usiri wa mikataba unavyoligharimu Tauifa akitolea mfano wa Mkataba wa ujenzi wa Bwawa la Umeme wa Julius Nyerere.

Amesema maeneo hayo yana changamoto nyingi ndiyo maana taasisi za uchunguzi zimekuwa zikiibua ubadhirifu mara kwa mara.

“Katika utekelezaji tumetangaziwa utamalizika baada ya miaka miwili ijayo lakini ndani ya mkataba ipo clear kuna bilioni 260 za CSR, na mkandarasi akichelewesha mkataba kwa mwaka mmoja anailipa Serikali asilimia 10. Sasa amechelewesha kwa miaka miwili tunamdai Sh 1.3 trilioni za kuchelewesha mkataba kwa miaka miwili kwanini kuna usiri?” amehoji Mpina.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!