MBUNGE wa Sengerema, Hamis Tabasamu ameibua “mambo mazito” bungeni kuhusu kuchezewa kwa tenda ya uagizaji wa mafuta ya Tarehe 18 Aprili 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Tabasamu ameibua hoja hiyo leo Alhamisi tarehe 28 Aprili, 2022 mara baada ya kipindi cha maswali na majibu ambapo aliomba kutoa hoja ya kuahirisha bunge na kujadadili suala hilo la dhararu.
Hata hivyo kabla ya kumaliza kueleza jambo hilo Spika Dk. Tulia Akson alimkatisha na kuhoji kama ameasilisha jambo hilo katika meza ya spika kutokana na uzito wa hoja yake.
Spika Tulia amesema hoja ya Tabasamu ni nzito na endapo ataacha ijadiliwe itaibua mambo mengi zaidi yatakayohitaji Ushahidi.
Leave a comment