Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Prof. Hoseah aanika mafanikio aliyofanya TLS, aomba achaguliwe tena
Habari Mchanganyiko

Prof. Hoseah aanika mafanikio aliyofanya TLS, aomba achaguliwe tena

Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), anayetetea kiti chake, Profesa Edward Hoseah
Spread the love

 

RAIS wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), anayetetea kiti chake, Profesa Edward Hoseah, amesema katika kipindi cha uongozi wake amefanikiwa kuimarisha mahusiano kati ya chama hicho na Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mgombea huyo urais wa TLS kwa awamu ya pili, ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 27 Aprili 2022, jijini Dar es Salaam, katika mdahalo wa wagombea urais wa chama hicho. Wengine ni, Jeremiah Mtobesya na Harold Sungusia.

Prof. Hoseah amesema, kufuatia kuimarika kwa mahusiano hayo, Serikali imekubali kutenga Sh. 1.4 bilioni, kwa ajili ya ruzuku kwa TLS katika utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria kwa wananchi.

“Nimeshaongea na Serikali nasubiri bajeti ambayo inaanza mwezi wa June, Wizara ya Katiba na Sheria imekubali kutenga Sh. 1.4 bilioni kwa ajili ya ruzuku katika zoezi la kusaidia misaada ya wananchi. Sababu TLS inatekeleza jukumu la umma,” amesema Dk. Hoseah.

Prof. Hoseah amesema, amefanikiwa kuishawishi Serikali kutenga fedha kwa ajili ya kusaidia uendeshaji wa Kituo cha Usuluhishi cha Kimataifa Tanzania, ambapo imekubali kutoa kiasi cha Sh. 1.2 bilioni.

“Serikali ilitaka migogoro ya kibiashara itatuliwe nchini, imekubali kutoa fedha kusaidia kituo Sh. 1.2 bilioni, ili tuweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na jambo hili sio geni, wale wanaofikiria kuhongwa na Serikali si sahihi,” amesema Prof. Hoseah.

Pia, Prof. Hoseah amesema katika kipindi cha uongozi wake amefanikiwa kuishawishi Mahakama Kuu ya Tanzania, kurejesha tozo za ada zinazotolewa na mawakili kiasicha Sh. 450, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati akigombea nafasi hiyo kwenye uchaguzi wa mwaka jana.

“Tumerudishiwa Sh. 450 milioni, ambazo tangu uhuru tulikuwa tukilipa mahakama kama ada, hatujawahi kurudishiwa. Kwa uongozi wangu zimetengwa Sh. 450 milioni, sasa jamani mnataka tufanyeje? Mimi sio wa blab la ni wa vitendo, nimetekeleza,” amesema Dk. Hoseah.

Akitaja mafanikio mengine, Prof. Hoseah amesema amefanikiwa kutekeleza ahadi yake ya kupunguza gharama ya bima ya afya, kutoka Sh. 1,050,000 hadi kufikia 500,000.

“Niliahidi mawakili wenye ulemavu kwamba tutashirikiana, niliahidi kuongea na mahakama katika mpango mkakati wa kuweka mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu na hili limetekelezwa na mahakama,” amesema Prof. Hoseah.

Prof. Hoseah amesema, amefanikiwa kupunguza tozo ya ada ya uwakili kutoka Sh. 60,000 hadi 20,000, huku akijinasibu kwamba, wakati wa uongozi wake hakuna wakili aliyefukuzwa au kusimamishwa kwa sababu mbalimbali.

Mgombea huyo Urais wa TLS, amewaomba mawakili wamchague ili aendelee na majukumu aliyoyaacha pamoja na mengine mapya aliyopanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!