Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watetezi haki za binadamu wafungua kesi ya dhamana kwa Madeleka
Habari MchanganyikoTangulizi

Watetezi haki za binadamu wafungua kesi ya dhamana kwa Madeleka

Spread the love

MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini (LHRC), wamefungua kesi ya kuomba dhamana ya Wakili Peter Madeleka, aliyekamatwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, tarehe 20 Aprili 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na THRDC, kesi hiyo Na. 16/2022, imefunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Kesi hiyo imefunguliwa na THRDC pamoja na LHRC, kupitia Mawakili, Mpale Kaba Mpoki, Jebra Kambole, Hassan Ruhanywa na Paul Kisabo, dhidi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI).

Washtakiwa wengine ni, Inspekta Jenerali wa Polisi nchini (IGP) na Afisa wa Makosa ya Jinai Kanda ya Dar es Salaam.

“THRDC kwa kushirikiana na LHRC wakiongozwa na mawakili wamefungua kesi ya kuomba dhamana mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Kesi imepangwa kusikilizwa Jumatatu, tarehe 25 Aprili 2022, saa sita kamili mchana mbele ya Hakimu Mfawidhi Kyaruzi,” imesema taarifa ya THRDC.

Madeleka alikamatwa na Jeshi la Polisi akiwa katika maeneo ya maegesho ya magari ya Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.

Mtandao huu ulimtafuta Wakili Kisabo, kwa njia ya simu leo Jumamosi, tarehe 23 Aprili 2022, kujua makosa anayotuhumiwa Wakili Madeleka, ambaye amesema hadi sasa haijulikana tuhuma zake.

“Hawajasema wanamshikilia kwa makosa gani , mimi wameninyima access ya kumuona. Sina taarifa kama amehojiwa au hajahojiwa, ningepewa taarifa ningejua amehojiwa kwa makosa gani,” amesema Wakili Kisabo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!