Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi hatarini kuondolewa UNHRC
Kimataifa

Urusi hatarini kuondolewa UNHRC

Spread the love

NCHI ya Urusi iko hatarini kuondolewa ujumbe katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC), kufuatia hatua yake ya kuivamia kijeshi Ukraine na kusababisha mauaji ya raia. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC, leo Alhamisi, tarehe 7 Aprili 2022, wanachama wa UN, wanatarajia kupiga kura ya kuamua kama Urusi inastahili kuondolewa UNHRC, kufuatia uvamizi wa kijeshi walioufanya Ukraine.

Katika mchakato wa huo, Urusi itaondolewa kama theluthi ya wajumbe wa UN watapiga kura ya ndiyo.

Azimio la kuitishwa kwa kura hiyo lilitolewa na nchi ya Marekani, kufuatia mauaji ya raia wa Ukraine, katika maeneo ya Bucha, kwenye Jimbo la Kyiv.

Urusi imepinga hatua hiyo ikidai ni ukiukwaji wa kanuni za UNHRC, utakaodhoofisha mfumo wa haki za binadamu wa baraza hilo.

Mkuu wa Urusi UN, Gennady Galitov, ameonya nchi watakaopiga kura hiyo, kuwa taifa lake litaihesabu kama adui yake.

“Kusimamishwa kwa haki ya Urusi kama mjumbe wa UNHRC, ni kudharau kanuni ya baraza, kuathiri ufanisi wake na kudhoofisha kabisa uaminifu, sio tu kwa haki za binadamu, lakini katika mfumo mzima wa hakiza binadamu wa UN,” amesema Gatilov.

Vita nchini Ukraine ilianza mwishoni mwa Februari 2022, baada ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin, kutangaza operesheni ya kijeshi nchini humo, ikiwa ni hatua ya kuishinikiza iache mpango wake wa kutaka kujiunga na Jumuiya ya Kujihami (NATO).

Mbali na Urusi kutaka Ukraine isijiunge na NATO, pia Taifa hilo linaunga mkono hatua ya waasisi wa mikoa ya mashariki ya nchi hiyo, kujitangazia uhuru na kutaka kuwa dola huru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!