Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yaja na mpango hifadhi ya mafuta ya kitaifa
Habari za Siasa

Serikali yaja na mpango hifadhi ya mafuta ya kitaifa

Spread the love

 

WAZIRI wa Nishati, January Makamba, amesema wizara yake imeandaa waraka wa uanzishwaji kanuni zitakazowezesha uundwaji wa hifadhi ya kimkakati ya kitaifa ya mafuta, ili kukabiliana na changamoto ya kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo katika soko la dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Makamba ametoa taarifa hiyo leo Jumanne, tarehe 6 Aprili 2022, jijini Dar es Salaam, akitoa ufafanuzi kuhusu changamoto ya mfumuko wa bei ya mafuta nchini.

Waziri huyo wa nishati amesema mabadiliko hayo ya kanuni yatapelekwa katika Bunge la Bajeti.

“Kumekuwa na kamati mbalimbali za kushughulikia suala la mafuta, ambayo kumekuwa na mapendekezo mbalimbali ya kuboresha na kuimarisha tasnia hii na bahati nzuri sisi tunafanyia kazi na kwenye Bunge la Bajeti tutatoa taarifa na muelekeo wa mambo mapya makubwa,” amesema Makamba.

January Makamba, Waziri wa Nishati

Makamba amesema “ikiwemo jambo ambalo kwa muda mrefu tumekuwa tunalitaka la hifadhi ya kimakakati ya taifa ya mafuta. Tumeandaa waraka ambao tutupeleka mbele kwa ajili ya uwezeshaji pamoja na kanuni mpya ya uanzishwa hifadhi hiyo, tuwe na uwezo wa kuhimili mabadiliko hayo.”

Amesema bei ya mafuta katika soko la dunia imepanda maradufu, ambapo bei ya petroli imepanda kutoka Dola za Marekani 561 kwa tani moja (2021), hadi kufikia dola 911, wakati dizeli bei yake ikipanda kutoka dola 503 hadi 823, katika kipindi hiko.

Makamba amesema kupanda kwa bei ya mafuta kulianza kusababishwa na janga la Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19), ulioibuka mwishoni mwa 2019, kisha ikachochewa zaidi ya mgogoro wa kivita kati ya Urusi na Ukraine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!