Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Meja Jenerali Urusi adaiwa kuuawa, Ukraine washangilia
Habari Mchanganyiko

Meja Jenerali Urusi adaiwa kuuawa, Ukraine washangilia

Spread the love

MAOFISA wa nchi za Magharibi pamoja Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ukraine, Anton Gerashchenko wamedai kuwa jenerali mwingine mwandamizi wa tatu ndani ya Jeshi la Urusi ameuawa nchini Ukraine. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Taarifa zinasema Jenerali Andrei Kolesnikov aliyetoka katika wilaya ya kijeshi ya mashariki mwa Urusi, ndiye aliyeuawa.

Kupitia akaunti yake ya Twitter Waziri huyo wa mambo ya ndani, amesema ni furaha iliyoje kuthibitisha kuwa Meja Jenerali watatu ameuawa katika mapambano hayo.

Awali jeshi la Ukraine lilisema Meja Jenerali Kolesnikov ambaye ni Kamanda wa jeshi la 29 la wilaya ya mashariki mwa Urusi, aliuawa.

Wachambuzi wa masuala ya kimataifa wamesema uwepo wa viongozi wa ngazi ya juu wa kijeshi ndani au karibu na uwanja wa vita inaweza kuwa ishara kwamba operesheni za Urusi haziendi kama zilivyopangwa.

Mbali na Kamanda huyo, Meja Jenerali mwingine ambaye anaingia katika kundi la viongozi wa ngazi za juu jeshini kuuawa ni Andrei Sukhovetsky aliyeuawa tarehe 2 Machi mwaka huu na kifo chake kuthibitishwa na Rais wa Urusi, Vladimir Putin.

Katika vita hiyo iliyoanza tarehe 24 Februari, mwaka huu inaelezwa kuwa wanajeshi kati ya 2000 hadi 4000 wa Urusi wameuawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa aanika mafanikio ya TMA

Spread the loveSHUGHULI za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), zimeimarika...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!