Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Madadapoa watangaza mgomo wa huduma kwa madereva bodaboda
Kimataifa

Madadapoa watangaza mgomo wa huduma kwa madereva bodaboda

Spread the love

BAADHI ya wanawake wanaofanya biashara haramu ya ngono katika Mji wa Mombasa nchini Kenya, wametangaza kusitisha kutoa huduma zao kwa waendesha bodaboda baada ya mwanamke mmoja nchini humo kushambuliwa na madereva hao katika barabara ya Wangari Maathai. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada madereva 16 kumvamia na kumnyang’anya Ofisa wa Ubalozi wa Zimbabwe nchini Kenya, simu yenye thamani ya Tsh milioni 2.6 na kumdhalilisha kijinsia.

Kutokana na tukio hilo lililoibua hisia kwa Wakenya wengi nchini humo, madadapoa hao wamesema wamechukua uamuzi huo kama ishara ya kukemea kitendo hicho.

Akinukuliwa na gazeti moja nchini humo, ‘Aisha’ ambaye sio jina lake halisi alisema kwamba wanabodaboda hawatafaidi huduma zake kwa wiki moja.

“Hawa watu ni wateja wangu ila kuanzia leo (tarehe 11 Machi, 2022), wiki moja kutoka sasa hawatapata nafasi ya kuonja raha,” alisema.

‘Aisha’ amesema hatua hiyo ni njia moja ya kudai haki kwa wanawake wote wanaonyanyaswa na kudhalilishwa mbele ya umma.

“Hii ndio sehemu inayonipa chakula cha kila siku, lakini nipo tayari kulala njaa ndiposa vitendo vya aina hii vikomeshwe,” aliongezea.

Tayari serikali kupitia kwa rais Uhuru Kenyatta ilitangaza kuwa wahudumu wote wa bodaboda watapatiwa mafunzo maalumu ili kurasimisha sekta hiyo.

Hata hivyo, tayari madereva hao 16 wamefikishwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Milimani jijini Nairobi, Gilbert Shikwe ambaye ameagiza watuhumiwa hao wabaki mahabusu hadi tarehe 24 Machi, mwaka huu.

Katika kesi hiyo iliyotajwa jana Hakimu huyo alisema “Polisi wanahitaji kupewa muda wa kutosha kukamilisha uchunguzi katika kesi hii iliyo na umuhimu mkubwa kwa umma.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!