Sunday , 12 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Blinken: NATO ipo tayari kama mzozo utatugusa
Kimataifa

Blinken: NATO ipo tayari kama mzozo utatugusa

Spread the love

 

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Kujihami-NATO, Jens Stoltenberg, amekutana na Katibu Mkuu wa Marekani, Antony Blinken pamoja na mawaziri wa mambo ya nje wa wanachama wa umoja huo Brussels nchini Ubelgiji, kwa lengo la kujadili hatua za kuchukua juu ya uvamizi wa Urusi nchini Ukreini. Inaripoti ABC News … (endelea).

Katika mkutano na waandishi wa habari kabla mkutano huo, Blinken na Stoltenberg alilaani mashambulizi yanayofanywa na Urusi kwa raia wa Ukreini na kutoa maoni juu ya ripoti ya mashambulizi katika mitambo ya nishati ya nyuklia.

“Hii ni ishara tu ya vita ya kizembe na umuhimu wa kuhakikisha inakoma na umuhimu wa Urusi kuondoa vikosi vyao vyote na kuunga mkono juhudi za kumaliza mzozo kwa diplomasia,” Stoltenberg amewaambia waandishi wa habari.

“Tunatoa misaada kwa Ukreini na wakati huo huo NATO si sehemu ya mzozo. NATO ni umoja wa kujihami, hatutafuti mzozo wa kivita na Urusi.”

Blinken alisisitiza kuwa NATO na Marekani “hazitaki mgogoro.”

“Lakini kama mzozo ukija kwetu, tupo tayari,” aliongeza “na tutalinda hata inchi moja ya mipaka yetu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!