Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Ummy akabidhi taulo za kike kampeni ya ‘Binti Ng’ara’
Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy akabidhi taulo za kike kampeni ya ‘Binti Ng’ara’

Spread the love

 

WAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu ametoa msaada wa taulo za kike paketi 1000 kwa Shirika lisilo la Kiserikali la Victoria Foundation kwa watoto wa kike waliopo shuleni, ambao hukumbwa na changamoto ya kushindwa kuhudhuria masomo kipindi cha hedhi jambo ambalo linalowarudisha nyuma kitaaluma. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Akikabidhi msaada huo kwa Mkurugenzi wa Shirika hilo katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya zilizopo jijini Dar es salaam leo tarehe 12 Februari, 2022, Ummy amesema amepata msukumo wa kutoa taulo hizo ili kuunga mkono kampeni ya “Binti Ng’ara, Timiza Malengo” inayotekelezwa na Victoria Foundation kwa ajili ya kuwasaidia mabinti wanaokosa uwezo wa kununua taulo hizo.

Waziri Ummy amesema kampeni ya Binti Ng’ara ni kampeni nzuri kwani imelenga kumuinua mtoto wa kike ambaye alikuwa anakosa taulo inayomwezesha kujistiri pindi anapokuwa kwenye siku zake.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Victoria Foundation, Vicky Kamata ameshukuru kwa msaada huo kutoka kwa Waziri Ummy na kusema utakuwa msaada mkubwa kwa watoto wa kike ambao wamekuwa wakishindwa kuhudhuria masomo yao kutokana na kuwa kwenye hedhi na hivyo kusubiri mpaka wamalize ndiyo waendelee na masomo.

Kamata ametoa ombi kwa wadau wengine kujitokeza katika kuchangia kampeni hiyo, ili kuweza kuwasaidia mabinti hao wanaokosa masomo pindi wanapokuwa kwenye hedhi, na kuweza kuwasaidia kuondokana na changamoto hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!