Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba: Nafasi yangu iko wazi 
Habari za Siasa

Prof. Lipumba: Nafasi yangu iko wazi 

Prof. Ibrahim Lipumba
Spread the love

 

MWENYEKITI  wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa. Ibrahim Lipumba, amesema nafasi yake iko wazi kwa yeyote atakayetaka kugombea kwenye uchaguzi wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika mwaka huu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Prof. Lipumba ametoa kauli hiyo leo Jumamosi, tarehe 12 Februari 2022, akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

“Natoa wito na kuwahakikishia wanachama kwamba, hii nafasi ya mwenyekiti iko wazi kwenye uchaguzi unaokuja, kwa maana kwamba kila mmoja anaweza kugombea nafasi hiyo,” amesema Prof. Lipumba.

Mwenyekiti huyo wa CUF, amesema lengo la kutoa kauli hiyo ni kuonesha kuwa hajawahi kuwa kikwazo kwa watu kugombea nafasi hiyo na kwamba kila mwanachama wa chama hicho anayo nafasi ya kugombea nafasi za juu za uongozi.

“Nasisitiza vijana wajitokeze kugombea nafasi zote ikiwa ni pamoja na nafasi ya mwenyekiti wa Taifa, kwamba Lipumba hajawa na hatokuwa kikwazo kwa watu kujitokeza kugombea nafasi hizo,” amesema – Prof.  Lipumba.

Aidha, Prof. Lipumba amesema anahitaji apate muda wa kukamilisha machapisho yake kuhusu ushiriki wake kwenye mapambano ya kudai haki, demokrasia na maendeleo ya uchumi wa Watanzania.

“Binafsi umri umekwenda Mingu akinijalia najitaji nipate muda wa kukamilisha machapisho ya ushiriki wangu katika mapambano ya kudai haki kwenye mapambano ya demokrasia na maendeleo ya uchumi wa Tanzania, wajibu wangu kuhakikisha chama kinakuwa imara na kupambana ili nchi yetu ipate haki,” amesema Prof. Lipumba.

Aidha, Prof. Lipumba amewaomba Watanzania waongeze ushiriki wao katika siasa ili wajenge demokrasia na vyama vya siasa vilivyo imara.

1 Comment

  • TZ TUNA MAHASIDI WA DEMOKRASIA HAWA (2) “LIPIMBA” NA “MREMA” HAO NDIO VIKWAZO VYA KUFIKI MALENGO YETU KAMA TAIFA TUKIWAACHA HAO VIPAKA SHUME HAMAD RASHI NA JOHN CHEYO.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!