SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco) limewaomba Watanzania kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho umeme unakatika kila mara kutokana na mvua na upepo mkali unaoharibu miundombinu yake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam .. . (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 22 Januari, 2022,kwa umma na Ofisi ya Uhusiano- Makao Makuu Dodoma, imesema upepo mkali na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha kwenye maeneo tofauti nchini, miundombinu ya umeme imeathirika kwa kiasi kikubwa.
Pia imesababisha baadhi ya wateja wao kukosa huduma ya umeme kwa nyakati tofauti.
“Tunawaomba uvumilivu wenu wapendwa wateja wakati mafundi wetu kote nchini wanaendelea na kazi ya kurekebisha miundombinu hiyo ili kurejesha huduma ya umeme. Tunaomba radhi wateja wetu kwa usumbufu unaojitokeza,” aimesema taarifa hiyo.
Leave a comment