Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko KAGAIGAI: Mifugo 1,257 imekufa Kilimanjaro kwa ukame
Habari Mchanganyiko

KAGAIGAI: Mifugo 1,257 imekufa Kilimanjaro kwa ukame

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai amesema jumla ya mifugo 1,257 imekufa mkoani humo kwa kukosa maji na malisho kutokana na ukame uliokumba mkoa huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea). 

Kagaigai ametoa kauli hiyo leo tarehe 22 Januari, 2022 wakati akitoa taarifa ya Mkoa huo kwa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amekwenda kuzindua Tamasha la Utamaduni mkoani humo.

Kagaigai ameitaja mifugo hiyo iliyokufa kuwa ni ng’ombe 841, kondoo 406 na punda 10

Amesema licha ya mafanikio na kazi mbalimbali za maendeleo zinazoendelea, mkoa huo unakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kutonyesha kwa mvua za vuli, hali ambayo imesababisha ukame na vifo vya mifugo.

“Uongozi wa mkoa unaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na hali hiyo. Pamoja na vifo hivyo vya mifugo, hali ya chakula bado ni nzuri, na Mkoa unachakula cha kutosha.

“Pamoja na ukame huo mkoa umejitosheleza kwa chakula hii ni kutokana na kuwa na ziada ya uzalishaji wa chakula tani 40,790 za wanga na tani 10,147 za mikunde zilizopatikana katika msimu nwa mvua 2020/2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!