Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua M/kiti NSSF, awapangia vituo mabalozi
Habari za Siasa

Rais Samia ateua M/kiti NSSF, awapangia vituo mabalozi

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Ali Idd Siwa, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), huku akiwapangaia vituo vya kazi mabalozi wanne. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo Jumamosi, tarehe 11 Desemba 2021 na
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Jaffar Haniu.

“Rais Samia amemteua Balozi Siwa, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya NSSF. Balozi Siwa ameteuliwa kwa kipindi cha pili kushika nafasi hiyo baada ya muda wa bodi hiyo kuisha tarehe 21 Septemba 2021,” imesema taarifa ya Haniu.

Pia, taarifa ya Haniu imewataja mabalozi waliopangiwa vituo vya kazi, akiwemo Balozi Said Shaib Musa, kuwa Balozi wa Tanzania nchini Kuwait na Balozi Fredrick Ibrahim Kibuta (Urusi).

Wengine ni, Balozi Said Juma Mshana (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo-DRC) na Balozi Alex Gabriel Kalua (Israel).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!