Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua M/kiti NSSF, awapangia vituo mabalozi
Habari za Siasa

Rais Samia ateua M/kiti NSSF, awapangia vituo mabalozi

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Ali Idd Siwa, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), huku akiwapangaia vituo vya kazi mabalozi wanne. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo Jumamosi, tarehe 11 Desemba 2021 na
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Jaffar Haniu.

“Rais Samia amemteua Balozi Siwa, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya NSSF. Balozi Siwa ameteuliwa kwa kipindi cha pili kushika nafasi hiyo baada ya muda wa bodi hiyo kuisha tarehe 21 Septemba 2021,” imesema taarifa ya Haniu.

Pia, taarifa ya Haniu imewataja mabalozi waliopangiwa vituo vya kazi, akiwemo Balozi Said Shaib Musa, kuwa Balozi wa Tanzania nchini Kuwait na Balozi Fredrick Ibrahim Kibuta (Urusi).

Wengine ni, Balozi Said Juma Mshana (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo-DRC) na Balozi Alex Gabriel Kalua (Israel).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!