RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewatembelea mawaziri wakuu wastaafu, Cleopa Msuya na Jaji Joseph Warioba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …(endelea).
Rais Samia amewatembelea viongozi hao wastaafu leo Alhamisi, tarehe 2 Desemba 2021, katika makazi yao kwa nyakati tofauti.
Picha zilizotolewa na Ikulu ya Tanzania, zinamwonesha Rais Samia akisalimia na kisha kuzungumza na Msuya na nyingine, akizungumza na Jaji Warioba.
Maelezo ya picha hizo, zinaeleza kwamba, Rais Samia amewatembelea wastaafu hao ni kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Tanzania Bara.
Kilele cha maadhimisho hayo, itakuwa tarehe 9 Desemba 2021, katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.
Leave a comment