Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bwege alazwa Muhimbili
Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Bwege alazwa Muhimbili

Suleiman Bungara 'Bwege'
Spread the love

 

ALIYEKUWA Mbunge wa Kilwa Kusini mkoani Lindi, Said Bungara ‘Bwege’, amelazwa katika wodi ya Sewahaji, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), akiugua kwa muda mrefu uvimbe kwenye shavu la kulia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Bwege alikuwa Mbunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Wananchi (CUF), kwa takribani miaka 10 ambapo uwakilishi wake ulivutia watu mbalimbali wa ndani na nje ya nchi. Mwaka 2020 aligombea kupitia ACT-Wazalendo na kushindwa.

Akizungumza na MwanaHALISI Online Bwege amesema amekuwa akisumbuliwa na uvimbe huo ulitokea kwenye shavu la kulia kwa muda mrefu, hali iliyomsababishia maumivu makali.

Bwege amesema uvimbe huo ulikuwa unamletea dalili za kupooza, hivyo ikamlazimu kwenda Hospitali ya Muhimbili kufanya uchunguzi na wiki iliyopita alifanyiwa upasuaji na madaktari bingwa wa hospitali hiyo.

Alishukuru madaktari waliomfanyia upasuaji huo, ambao ulikwenda vizuri na kwamba ni matumaini yake atatoka mapema.

“Ni kweli nimelazwa hapa Muhimbili na juzi nilifanyiwa upasuaji ambao ulikwenda salama na kwa sasa nadiriki kusema naendelea vizuri, Mungu akipenda nitatoka madaktari wakiamua,” amesema.

Mbunge huyo wa zamani ambaye amejitengenezea umaarufu kwa kupigania haki za wapiga kura wake, amesema tangu afanyiwe upasuaji anaendelea vizuri.

Aidha, Bwege ambaye amekuwa maarufu kutokana na misemo yake iliyojaa vichekesho, alisema tofauti na changamoto hiyo aliyokutana nayo, pia anasumbuliwa na kisukari.

Bwege ameomba wananchi wamwombee ili afya yake iweze kutengamaa na aweze kuendelea kupigania nchi kama kawaida yake.

“Nimekuwa nikifanya kazi ya siasa kila siku na tatizo hili nilikuwa nalo, lakini baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, nimekuja Muhimbili, nashukuru kuwa dalili za kuendelea kujenga nchi kupitia siasa zitaendelea,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa aanika mafanikio ya TMA

Spread the loveSHUGHULI za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), zimeimarika...

error: Content is protected !!