Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba ni mwendo wa Tik-taka, waapa kuichakaza Yanga
Michezo

Simba ni mwendo wa Tik-taka, waapa kuichakaza Yanga

Mwenyekiti wa Bodi ya Simba, Salim Abdallah ‘Try Again
Spread the love

 

KLABU ya Soka ya Simba imeapa kuondoka na ushindi kwenye mchezo watani wa jadi wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Yanga kwa kuwa timu yao kwa sasa ipo vizuri. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa mzunguko wa kwanza, ambao Simba ndiyo watakuwa wenyeji utapigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa, tarehe 11, Novemba 2021 majira ya saa 11 jioni.

Akizungumza kwenye mkutano Mkuu wa mwaka wa klabu hiyo, uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere, Mwenyekiti wa bodi ya klabu hiyo Salim Abdallah ‘Try Again’ amesema kuwa wanasimba kwa sasa wanakila sababu ya kutembea kifua mbele, kwa kuwa timu yao ipo kwenye mikono salama.

Wanasimba mnakila sababu ya kutembea kifua mbele msiwe wanyonge, Simba ipo kwenyre mikono salama, watake wasitake mpira utachezwa mmeona juzi Mwanza, sisi ni Tik-taka tu,” alisema Try Again.

Aidha mwenyekiti huyo wa bodi, aliendelea kusema kuwa wao ndiyo wenyeji wa mchezo huo na aliwahakikishia wanachama hao kuwa wataifunga Yanga kwa kuwa mbinu zao zote wanazijua.

“Tarehe 11, mwezi ujao tunashughuli pale sisi ndio wenyeji nataka tuwahakikishieni tutawapiga, mipango yote tunaijua mbinu zote tunazijua,” aliongezea.

Katika hatua nyingine kiongozi huyo alisema kuwa Simba kwa sasa imewekeza kwenye mpira na siyo kuwekeza kwenye vijembe kwa kuwa wao ni moja ya klabu 10 bora barani Afrika.

Simba imewekeza kwenye mpira, Simba haijawekeza kwenye kejeri fitna na vijembe, huku tumeshapita, ndani ya klabu 10 bora Afrika Simba tumo hao wengine sijui ya ngapi,” alisema Try Again.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!