Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bwege alazwa Muhimbili
Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Bwege alazwa Muhimbili

Suleiman Bungara 'Bwege'
Spread the love

 

ALIYEKUWA Mbunge wa Kilwa Kusini mkoani Lindi, Said Bungara ‘Bwege’, amelazwa katika wodi ya Sewahaji, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), akiugua kwa muda mrefu uvimbe kwenye shavu la kulia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Bwege alikuwa Mbunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Wananchi (CUF), kwa takribani miaka 10 ambapo uwakilishi wake ulivutia watu mbalimbali wa ndani na nje ya nchi. Mwaka 2020 aligombea kupitia ACT-Wazalendo na kushindwa.

Akizungumza na MwanaHALISI Online Bwege amesema amekuwa akisumbuliwa na uvimbe huo ulitokea kwenye shavu la kulia kwa muda mrefu, hali iliyomsababishia maumivu makali.

Bwege amesema uvimbe huo ulikuwa unamletea dalili za kupooza, hivyo ikamlazimu kwenda Hospitali ya Muhimbili kufanya uchunguzi na wiki iliyopita alifanyiwa upasuaji na madaktari bingwa wa hospitali hiyo.

Alishukuru madaktari waliomfanyia upasuaji huo, ambao ulikwenda vizuri na kwamba ni matumaini yake atatoka mapema.

“Ni kweli nimelazwa hapa Muhimbili na juzi nilifanyiwa upasuaji ambao ulikwenda salama na kwa sasa nadiriki kusema naendelea vizuri, Mungu akipenda nitatoka madaktari wakiamua,” amesema.

Mbunge huyo wa zamani ambaye amejitengenezea umaarufu kwa kupigania haki za wapiga kura wake, amesema tangu afanyiwe upasuaji anaendelea vizuri.

Aidha, Bwege ambaye amekuwa maarufu kutokana na misemo yake iliyojaa vichekesho, alisema tofauti na changamoto hiyo aliyokutana nayo, pia anasumbuliwa na kisukari.

Bwege ameomba wananchi wamwombee ili afya yake iweze kutengamaa na aweze kuendelea kupigania nchi kama kawaida yake.

“Nimekuwa nikifanya kazi ya siasa kila siku na tatizo hili nilikuwa nalo, lakini baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, nimekuja Muhimbili, nashukuru kuwa dalili za kuendelea kujenga nchi kupitia siasa zitaendelea,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!