Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hati ya ukamatiji yaibu mvutano kesi ya Mbowe, yaahirishwa
Habari za SiasaTangulizi

Hati ya ukamatiji yaibu mvutano kesi ya Mbowe, yaahirishwa

Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi jijini Dar es Salaam, imeahirisha usililizwaji wa kesi inayomkabili, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake hadi kesho Jumanne, tarehe 9 Novemba 2021. Anariooti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ni ili iandae uamuzi wa pingamizi la upande wa utetezi dhidi ya hati ya uchukuaji mali ya washtakiwa wawili katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi yenye mashtaka ya kupanga njama za vitendo vya kigaidi.

Kesi hiyo imeahirishwa leo Jumatatu, tarehe 8 Novemba 2021 na mahakama hiyo mbele ya Jaji Joackim Tiganga, baada ya kuibuka mvutano kati ya mawakili wa jamhuri na utetezi kuhusu pingamizi hilo.

Hati hiyo inayopingwa ni ya uchukuaji mali za washtakiwa wawili, Adam Kasekwa na Mohammed Abdllah Ling’wenya, waliokamatwa maeneo ya Rau Madukani, Moshi mkoani Kilimanjaro, tarehe 5 Agosti 2020.

Ambayo ililetwa mahakamani hapo leo na Mkuu wa Upelelezi Wilayani Arumeru, Arusha, SP Jumanne Malangahe, akitoa ushahidi wake namna alivyowapekuwa washtakiwa hao, baada ya kukamatwa kwa kosa la kula njama za kufanya vitendo vya ugaidi.

Jaji Tiganga ameahirisha usikilizwaji wa kesi hiyo hadi kesho tarehe 9 Novemba 2021, atakapotoa uamuzi wa mahakama hiyo dhidi ya hati ya uchukuaji mali za washtakiwa hao, kama itapokelewa au haitapokelewa.

“Nikitazama muda sidhani kama nitaweza kamilisha uamuzi, naomba niahirishe mpaka kesho saa 3.00 asubuhi,” amesema Jaji Tiganga.

Mvutano huo wa kisheria uliibuka baada ya upande wa utetezi kuweka pingamizi hilo, ukidai hati hiyo limeletwa mahakamani hapo chini ya kifungu cha sheria ambacho hakipo.

Wakili wa utetezi, Nashon Nkungu, amedai kifungu cha 38 (3) cha Sura ya 20 ya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, iliyofanyiwa marekebisho 2018, kilichotumika katika hati hiyo, hakipo katika sheria za nchi, kwa kuwa sheria hiyo haikufanyiwa marekebisho mwaka huo bali ilirekebishwa 2019.

Lakini upande wa jamhuri kupitia Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando, umepinga hoja hizo ukidai kwamba hazina mashiko kwa mujibu wa Sheria ya Kutafsiri Sheria.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!