Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wazee CUF wamkingia kifua Profesa Lipumba
Habari za Siasa

Wazee CUF wamkingia kifua Profesa Lipumba

Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mohamed Chunga
Spread the love

 

JUMUIYA ya Wazee wa chama cha upinzani cha wananchi nchini Tanzania (CUF), kimeonya wale wote wanaoendesha vuguvugu la kumng’oa kwenye nafasi hiyo, Profesa Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa chama hicho kuacha mara moja. Anaripoti Victoria Mwakisimba TUDARCo … (endelea).

Wazee hao wameibuka kumtetea Profesa Lipumba baada ya kuwapo na mikakati ya kumtaka kujiuzulu wakipinga kile anachokifanya mwenyekiti huyo cha kutengua baadhi ya waliokuwa wakurugenzi mbalimbali wa chama hicho na kuteua wapya.

Leo Alhamisi, tarehe 23 Septemba 2021, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mohamed Chunga amezungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya CUF, Buguruni jijini Dar es Salaam akisema, hatokubali kuona mipango hiyo ikitekelezwa.

Chunga amesema, katiba ya chama ya mwaka 2019 inampa mamlaka mwenyekiti kuteua na kutengua kiongozi hasa pale anapokwenda kinyume na maadili, kukihujumu chama, kushindwa kuwajibika katika nafasi aliyopewa na kwenda kinyume na katiba ya chama.

Amesema kumezuka maneno ya kumtukana mwenyekiti wao ambayo yanaenezwa na baadhi ya wanachama na viongozi wachache huku wakitaka mwenyekiti wao kuachia ngazi hiyo.

Chunga amesema kwa takribani miaka minne chama kimekuwa kwenye mgogoro ambao ulitengenezwa kwa makusudi wakidai Profesa Lipumba sio mwenyekiti wa chama hicho kwa kuwa alijiuzulu mwenyewe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!