Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wazee CUF wamkingia kifua Profesa Lipumba
Habari za Siasa

Wazee CUF wamkingia kifua Profesa Lipumba

Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mohamed Chunga
Spread the love

 

JUMUIYA ya Wazee wa chama cha upinzani cha wananchi nchini Tanzania (CUF), kimeonya wale wote wanaoendesha vuguvugu la kumng’oa kwenye nafasi hiyo, Profesa Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa chama hicho kuacha mara moja. Anaripoti Victoria Mwakisimba TUDARCo … (endelea).

Wazee hao wameibuka kumtetea Profesa Lipumba baada ya kuwapo na mikakati ya kumtaka kujiuzulu wakipinga kile anachokifanya mwenyekiti huyo cha kutengua baadhi ya waliokuwa wakurugenzi mbalimbali wa chama hicho na kuteua wapya.

Leo Alhamisi, tarehe 23 Septemba 2021, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mohamed Chunga amezungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya CUF, Buguruni jijini Dar es Salaam akisema, hatokubali kuona mipango hiyo ikitekelezwa.

Chunga amesema, katiba ya chama ya mwaka 2019 inampa mamlaka mwenyekiti kuteua na kutengua kiongozi hasa pale anapokwenda kinyume na maadili, kukihujumu chama, kushindwa kuwajibika katika nafasi aliyopewa na kwenda kinyume na katiba ya chama.

Amesema kumezuka maneno ya kumtukana mwenyekiti wao ambayo yanaenezwa na baadhi ya wanachama na viongozi wachache huku wakitaka mwenyekiti wao kuachia ngazi hiyo.

Chunga amesema kwa takribani miaka minne chama kimekuwa kwenye mgogoro ambao ulitengenezwa kwa makusudi wakidai Profesa Lipumba sio mwenyekiti wa chama hicho kwa kuwa alijiuzulu mwenyewe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!