JUMUIYA ya Wazee wa Chama cha Wananchi (CUF) imemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kufufua mchakato wa Katiba mpya pamoja na kuruhusu mikutano ya hadhara ili kurejesha haki kwa vyama vya siasa nchini kutekeleza majukumu yao kikamilifu. Anaripoti Noela Shila – TUDARCo … (endelea).
Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 23 Septemba, 2021 na Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Mohammed Chunga wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu madai mbalimbali ya chama hicho.
Pia mwenyekiti huyo ameungana na vyama vingine vya siasa kumuomba Rais Samia afufue mchakato wa katiba mpya ili ipatikane Tume Huru ya Uchaguzi nchini.
Amesema kitendo cha kuzuia mikutano ya hadhara ni ukiukwaji wa katiba ya nchi ambayo viongozi wameapa kuilinda.
“Maandamano ni haki ya vyama vya siasa kwa mujibu wa katiba ya nchi ndio maana tunasisitiza viongozi waheshimu katiba.
“Tunaamini mikutano ya hadhara ikirejeshwa, mvutano kati ya polisi na vyama vya siasa ambao umejitokeza katika kipindi cha miaka mitano iliypota hautoendelea,” amesema.
Leave a comment