Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kisa bintiye kunyolewa nywele… mzazi adai fidia ya Sh bilioni 2.3
Kimataifa

Kisa bintiye kunyolewa nywele… mzazi adai fidia ya Sh bilioni 2.3

Spread the love

 

BABA mmoja raia wa Marekani amedai alipwe dola milioni moja sawa na Sh bilioni 2.3 baada ya binti yake mwenye umri wa miaka saba kunyolewa nywele na mwalimu wake. Anaripoti Noela Shilla TUDARCo … (endelea).

Jimmy Hoffmeye ameishtaki shule anayosoma mtoto wake pamoja na wafanyakazi wake wawili kwa kumnyoa binti yake bila ruhusa ya mzazi.

Kwa mujibu wa mashtaka yake, Hoffmeyer amesema haki ya mtoto wake ya kuwa na nywele ilikiukwa na ameamua kumhamisha mtoto wake katika shule hiyo.

Uchunguzi uliofanywa kuhusiana na kisa hicho, ulibaini kuwa licha ya kumnyoa nywele, mwalimu huyo pia alimbagua kwa misingi ya rangi yake.

Mwalimu huyo alipatikana na hatia lakini aliendelea kufanya kazi katika shule ya Ganiard iliyopo Michigan.

Mashtaka dhidi ya shule na wafanyakazi wake wawili kumhusi bintiye yalipelekewa katika Mahakama ya Michigan nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Bunge kumuweka katibu mkuu wa EAC kikaangoni

Spread the loveAliyekuwa Katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dk. Peter...

Kimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

error: Content is protected !!