Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ecowas yaisimamisha Guinea uanachama
Kimataifa

Ecowas yaisimamisha Guinea uanachama

Spread the love

 

JUMUIYA ya kiuchumi ya nchi za Afrika magharibi ECOWAS imesimamisha uanachama wa Guinea baada ya wanajeshi wa nchi hiyo kuiangusha serikali ya Rais Alpha Conde.  Anaripoti Mwandishi Wetu …  (endelea).

Jumuiya ya ECOWAS imeitaka Guinea irejee kwenye utaratibu wa kawaida wa katiba.

Kutokana na hatua hiyo Guinea kwa sasa imesimamishwa kwenye mabaraza yote ya kupitisha maamuzi ya jumuiya hiyo.

Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika magharibi pia imetoa mwito kwa Guinea wa kuanzisha mchakato wa kurejea haraka kwenye uongozi wa kikatiba.

Waziri wa mambo ya nje wa Burkina Faso, Alpha Barry

Waziri wa mambo ya nje wa Burkina Faso, Alpha Barry amesema baada ya mkutano wa viongozi wa nchi 15 za ECOWAS kwamba jumuiya hiyo inataka kuachiwa huru mara moja kwa rais Alpha Conde aliyekamatwa na wanajeshi waliotwaa madaraka.

Ujumbe wa upatanishi wa jumuiya ya ECOWAS unatarajiwa kuwasili leo tarehe 9 Septemba katika mji mkuu wa Guinea, Conakry.

Umoja wa Mataifa pamoja na Umoja wa Afrika pia zimelaani mapinduzi ya kijeshi nchini Guinea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!