SARE ya bao 1-1, ilitosha kuifanya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kuondoka na pointi moja kwenye mchezo wa kusaka tiketi ya fainali za kombe la Dunia dhidi ya Jamhuri ya Congo. Anaripoti Mintanga Hunda, TUDARCo
Fainali hizo zitachezwa nchini Qatar 2022, ambapo kwenye mchezo wa kwanza wa kundi J, uliopigwa nchini Congo, kwenye dimba la TP Mazembe Stars ilitoshana nguvu na wenyeji hao.
Kwenye mchezo huo, Congo walikuwa wa kwanza kupata bao kwenye dakika ya 22, kupitia kwa Dieumerci Mbokani na dakika 15 baadae Stars walichomoa bao hilo, kupitia kwa Simon Msumva kwenye dakika ya 37, kwa shuti kali nje ya 18.
Stars ambayo ipo chini ya kocha Kim Poulsen iliingia kwenye mchezo huo, huku likikosekana jina la nahodha wake Mbwana Samatta ambaye alichelewa kujiunga na timu hiyo.
Samatta hakulipoti kikosi toka timu hiyo ilipoingia kambini Agosti 24, mwaka huu jijini Dar es Salaam, na kufanya maandalizi kwa siku tano kabla ya kufasiri Agosti 31 kuelekea nchini Congo.
Kwa matokeo hayo Stars inajiweka kwenye nafasi nzuri ndani ya kundi J, kuelekea mchezo wa pili dhidi ya Madascar utakaopigwa Septemba 7, 2021 kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
Stars itarejea nchini kesho kwa ndege ya kukodi ya shirika la ndege la Air Tanzania na kuingia kambini moja kwa moja kujianda na mchezo huo wa Madagascar.
Leave a comment