Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Baba mkwe amtaka Waziri asitumie jina la Gwajima
Habari MchanganyikoTangulizi

Baba mkwe amtaka Waziri asitumie jina la Gwajima

Spread the love

MZEE Mathias Gwajima, Baba mkwe wa Waziri wa Afya, Dk. Dorothy Gwajima, amemtaka mkamwana wake huyo aache kutumia jina lake la ukoo kwa madai kwamba anaiharibu familia yake baada ya kuagiza vyombo vya dola vimkamate shemeji yake, Askofu Josephata Gwajima. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ombi hilo imetolewa na Mzee Gwajima, leo Jumapili, tarehe 22 Agosti 2021, akiongea mbele ya Askofu Gwajima, katika Kanisa la Ufufuo na Uzima, siku chache baada ya Dk. Gwajima kuviagiza vyombo vya dola vimhoji shemeji yake, ili athibitishe madai yake dhidi ya chanjo ya ugonjwa wa Korona (UVIKO-19).

Akizungumza kanisani hapo, Mzee Gwjaima amemuomba Dk. Gwajima ambaye ameolewa na mdogo wake Askofu Gwajima atumie jina lingine.

“Mimi namuomba bwana mdogo achukue njia nyingine, jina la Gwajima alifute kabisa. Achukue jina lingine, mimi sielewi sasa anafikiri kitu gani, yeye kama anajifanya kwamba ana akili ya kutosha basi ajitenge na mimi,” amesema Mzee Gwajima.

Mzee Gwajima ameongeza “Mimi kwa kweli usemi sina isipokuwa sasa huyu mama yetu huyu anajiita Gwajima, nasikitika sana na mimi ningekuomba hata jina la Gwajima asingelitumia, anataka kuniharibia familia yangu.”

Mzee Gwajima ametoa msimamo huo, baada ya Askofu Gwajima ambaye ni Mbunge wa Kawe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumuomba ridhaa baba yake akimtaka amruhusu ampasue pasue waziri huyo wa afya, kufuatia agizo lake la kutaka akamatwe.

“Sasa nataka nimpasue pasue vipande vipande, ila sasa kwa sababu ni mkweo sitaki wewe ukasirike. Sasa mzee unasemaje?” amesema Askofu Gwajima.

1 Comment

  • Mmmmh!

    Mambo haya ni kazi sana. Kutoka uwajibikaji hadi kwenye familia.

    Mambo ya korona hadi kukamatwa. Yote kwa yote kila jambo lina mwisho wake.

    Kila aliyeumia kwenye jambo hili maumivu yake yatapita.

    Hisia zetu wanadamu ni kama mawimbi ya bahari kuna wakati yanakuwa makali na ya kutisha kuna wakati yanakuwa vivutio kwa watu.

    Hisia zina mzunguko, leo una huzuni kesho haieleweki kuwa huzuni itaondoka au la.

    Lakini mara zote hisia huwa na mzunguko. Leo utakuwa na furaha kesho inaweza kuwa tofauti.

    Rafiki yako,

    Aliko Musa.

    Mbobezi Kwenye Majengo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!