Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kina Mbowe wasomewa mashtaka upya, DPP hajakamilisha taratibu
Habari za SiasaTangulizi

Kina Mbowe wasomewa mashtaka upya, DPP hajakamilisha taratibu

Freeman Mbowe akiwa mahakamani
Spread the love

 

KIONGOZI wa chama kikuu cha upinzania nchini Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu, wamesomewa upya mashtaka katika kesi ya ugaidi inayowakabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mbowe na wenzake wamesomewa mashtaka hayo upya leo Ijumaa tarehe 6 Agosti 2021, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na afisa kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtka nchini humo (DPP), Pius Hilla.

Hakimu Simba, ametoa uamuzi huo kwa kuwa washtakiwa hao walisomea mashtaka wakiwa tofauti. Mbowe ambaye ni mshhtakiwa wa nne ameunganishwa katika kesi hiyo iliyofunguliwa mwaka 2020.

Hata hivyo, washtakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na mamlama ya kusikiliza mashtaka ya ugaidi na uhujumu uchumi yanayowakabili.

Mbali na mbowe, washtakiwa wengine; ni Halfani Bwire Hassan, Adam Hassan Kasekwa na Mohammed Abdillahi Lingwenya.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 13 Agosti 2021 baada ya upande wa Jamhuri kudai ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hijakamilisha taratibu za kuifungua kesi hiyo kwenye mahakama yenye mamlaka ya kusikiliza ambayo ni Mahakama Kuu.

Mbowe na wenzake, wamesomewa mashitaka matano, shtala la kwanza ni kula njama za kufanya ugaidi linawakabili wote wanne, ambapo wanadaiwa kwenda kinyume na sheria ya kuzuia ugaidi na uhujumu uchumi.

Wanadaiwa kutenda kosa hilo kati ya tarehe 1 Mei na 1 Agosti 2020 katika maeneo mbalimbali, ikiwemo Hotel ya Aishi mkoani Kilimanjaro. Mkoani Dar es Salaam, Morogoro na Arusha.

Kosa la pili linamkabili Mbowe pekee, anadaiwa kufadhili vitendo vya ugaidi kwa kutoa fedha za kufadhili ugaidi. Mbowe anadaiwa kutenda kosa hilo 1 Agosti 1 2020 akiwa katika hoteli ya Aishi.

Shtaka la tatu, linamkabili Adam la kumiliki silaha kinyume cha sheria anadaiwa kutenda kosa hilo tarehe 5 Agosti mwaka 2020 ambapo alikutwa na silaha aina ya Pisto.

Shtaka la nne linamkabili pia adam la kupatikana na risasi tatu pasipokuwa na leseni na sla tano linamkabili Halfani la kukutwa na sare na vifaa vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), anadaiwa kutenda kosa hilo tarehe 10 Agosti 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!