Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Baraza la NGO’s laomba kuonana na Rais Samia
Habari Mchanganyiko

Baraza la NGO’s laomba kuonana na Rais Samia

Spread the love

 

BARAZA la Taifa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s), nchini Tanzania- NACONGO, limeomba kufanya mazungumzo na Rais Samia Suluhu Hassan, ili kutafuta suluhu ya changamoto zinazozikabili mashirika hayo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Ombi hilo limetolewa jana tarehe 9 Julai 2021, jijini Dodoma na Mwenyekiti wa NACONGO, Lilian Joseph Badi, baada ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo, kupitia uchaguzi wa baraza hilo uliofanyika juzi jijini humo.

Lilian aliomba kukutana na Rais Samia, ili wajadili namna ya kuweka mikakati ya ushirkiano baina ya mashirika hayo na Serikali yake, hususan katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi.

Rais wa Tanzania,
Samia Suluhu Hassan

Aidha, Lilian alisema baraza hilo litahakikisha linaleta umoja kati ya NGO’s, wadau na Serikali, ili kuhakikisha utekelezaji wa mipango mikakati iliyowekwa na Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo, inafanikiwa.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Idara Kuu ya Maendeleo Jamii, Patrick Golwike, alilitaka baraza hilo kufanya kazi kwa kuzingatia sheria za nchi.

Ili kuisaidia Serikali katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi, kwenye kujiletea maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!