Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Dar ayapa masharti mabasi yaendayo mikoani
Habari Mchanganyiko

RC Dar ayapa masharti mabasi yaendayo mikoani

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla, ameagiza wamiliki wa mabasi yaendayo mkoani, wafuate utaratibu wa kupakia na kushusha abiria katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Mbezi Luis. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Makalla ametoa agizo hilo leo Ijumaa, tarehe 9 Julai 2021, alipotembelea kituo hicho kilichopo wilayani Ubungo mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam, ameliagiza Jeshi la Polisi lisimamie utekelezwaji wa malekezo hayo.

“Hiki ndiyo kituo kikubwa cha mabasi, mimi kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama naagiza hiki ndio kituo unapoingia Dar es Salaam, mabasi yote yatapita hapa yatakuja katika kituo hiki Jeshi la Polisi lisimamie maelekezo haya,” amesema Makalla.

Makalla amesema Serikali inatambua kituo kimoja cha mabasi,  hivyo hakuna maana kama kila mmiliki wa mabasi atakuwa na kituo chake cha kupakia na kushusha abiria.

Aidha, RC Makalla ameelekeza uongozi wa kituo hicho kuweka utaratibu wa baadhi ya mabasi kushusha abiria kwenye eneo la kulaza magari,  ambalo lina mabanda ya mamalishe ili kuchochea biashara zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!