Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Dar ayapa masharti mabasi yaendayo mikoani
Habari Mchanganyiko

RC Dar ayapa masharti mabasi yaendayo mikoani

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla, ameagiza wamiliki wa mabasi yaendayo mkoani, wafuate utaratibu wa kupakia na kushusha abiria katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Mbezi Luis. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Makalla ametoa agizo hilo leo Ijumaa, tarehe 9 Julai 2021, alipotembelea kituo hicho kilichopo wilayani Ubungo mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam, ameliagiza Jeshi la Polisi lisimamie utekelezwaji wa malekezo hayo.

“Hiki ndiyo kituo kikubwa cha mabasi, mimi kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama naagiza hiki ndio kituo unapoingia Dar es Salaam, mabasi yote yatapita hapa yatakuja katika kituo hiki Jeshi la Polisi lisimamie maelekezo haya,” amesema Makalla.

Makalla amesema Serikali inatambua kituo kimoja cha mabasi,  hivyo hakuna maana kama kila mmiliki wa mabasi atakuwa na kituo chake cha kupakia na kushusha abiria.

Aidha, RC Makalla ameelekeza uongozi wa kituo hicho kuweka utaratibu wa baadhi ya mabasi kushusha abiria kwenye eneo la kulaza magari,  ambalo lina mabanda ya mamalishe ili kuchochea biashara zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!