Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Mwamakula aitahadharisha CCM
Habari za Siasa

Askofu Mwamakula aitahadharisha CCM

Askofu Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania na Afrika Mashariki, Emmaus Mwamakula
Spread the love

 

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania na Afrika Mashariki, Emmaus Mwamakula, amekishauri Chama Cha Mapinduzi (CCM), kisikatae marekebisho ya katiba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Askofu Mwamakula ametoa ushauri huo leo Alhamisi tarehe 1 Julai 2021, katika uzinduzi wa kongamano la kidai katiba mpya, lililoandaliwa na Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jijini Dar es Salaam.

“Waliokuwa kwenye madaraka sasa naomba watuelewe, hili jambo litawageuka na kama watakataa kubadili katiba kuna uwezekano upinzani kuingia madarakani kwa kutumia katiba hii na wakiitumia kulipiza kisasi itakuwa ole kwao, wataumia sana,” amesema Askofu Mwamakula.

Askofu Mwamakula amesema, endapo chama cha upinzani kitaingia madarakani kupitia katiba hiyo, CCM kitaathirika na mapungufu ya katiba hiyo.

“Tunataka tuwaambie wanaotawala kwamba katiba hii tunayoipinga, endapo wapinzani wakiingia kwa katiba hii watakwisha wote, lakini tukiibadilisha tutakuwa na kuheshimiana huko mbele,” amesema Askofu Mwamakula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!