Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Mwamakula aitahadharisha CCM
Habari za Siasa

Askofu Mwamakula aitahadharisha CCM

Askofu Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania na Afrika Mashariki, Emmaus Mwamakula
Spread the love

 

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania na Afrika Mashariki, Emmaus Mwamakula, amekishauri Chama Cha Mapinduzi (CCM), kisikatae marekebisho ya katiba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Askofu Mwamakula ametoa ushauri huo leo Alhamisi tarehe 1 Julai 2021, katika uzinduzi wa kongamano la kidai katiba mpya, lililoandaliwa na Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jijini Dar es Salaam.

“Waliokuwa kwenye madaraka sasa naomba watuelewe, hili jambo litawageuka na kama watakataa kubadili katiba kuna uwezekano upinzani kuingia madarakani kwa kutumia katiba hii na wakiitumia kulipiza kisasi itakuwa ole kwao, wataumia sana,” amesema Askofu Mwamakula.

Askofu Mwamakula amesema, endapo chama cha upinzani kitaingia madarakani kupitia katiba hiyo, CCM kitaathirika na mapungufu ya katiba hiyo.

“Tunataka tuwaambie wanaotawala kwamba katiba hii tunayoipinga, endapo wapinzani wakiingia kwa katiba hii watakwisha wote, lakini tukiibadilisha tutakuwa na kuheshimiana huko mbele,” amesema Askofu Mwamakula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!